Friday 17 June 2016

Kutoka Bungeni June 16, 2016: Idadi ya Wabunge Waliosimamishwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge Yaongezeka..

Kamati ya bunge imejadili na kuamua kuwasimamisha wabunge wawili wa Chadema baada ya kutoa taarifa za uongo ndani ya bunge, wabunge hao ni pamoja na Susan Lymo na Anatropia Theonest.
Katika bunge hilo lilofanyika June 16, Mbunge Susan Lymo ambae amesimamisa vikao kuanzia June 17 hadi 24, alilidanganya bunge baada ya kusema kuwa Jeshi la Polisi Limenunua Magari 777 ya washawasha ikiwa ni idadi ya magari ambayo yamepangwa kuingizwa na jeshi hilo kwa matumizi mbalimbali.
Nae Anatropia Theonest alilidanya bunge baada ya kusema kuwa waziri wa ardhi na nyumba William Lukuvi alichukua ardhi ya wananchi akiwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Hivyo kamati ya bunge kuamua kumsimamisha kutohudhuria vikao vitatu vya bunge.

Follow us on our facebook page; Kwetutz24.com and follow us on twitter: @kwetutz24 and Pininterest: @kwetutz24 

Related Posts

Kutoka Bungeni June 16, 2016: Idadi ya Wabunge Waliosimamishwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge Yaongezeka..
4/ 5
Oleh
Show Comments: OR