Tuesday 14 June 2016

POLISI WOTE NCHINI KUKUMBWA NA ADHABU HII...


Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo, na Uvuvi Willium Ole Nasha amesema kuwa Serikali Imetangaza adhabu ya kuwakata mishahara na adhabu nyingine, askari Polisi wote nchini ambao hawata wapigia saluti wabunge wa Bunge la Muungano na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Alisema haya wakati akijibu swali kutoka kwa mbunge wa viti Maalum (CCM) Fakharia Khamis, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Na kuongeza kuwa Askari yoyote ambae hatotoa saluti ataripotiwa kwa kiongozi wake ambapo atapewa adhabu ikiwemo kukatwa mshahara, kupigishwa paredi na adhabu nyinginezo.
Naibu huyo pia alisema kuwa sheria hiyo imetajwa kwa vyeo vyote kuwa wanatakiwa kupiga saluti kwa Rais wa Bara na Zanzibar, kwa makamu wote  wa Rais wa Zanzibar  na wengineyo kama Spika.

Related Posts

POLISI WOTE NCHINI KUKUMBWA NA ADHABU HII...
4/ 5
Oleh
Show Comments: OR