Saturday 28 May 2016

Rais Wa Somalia Ataka Njia Muafaka kuwarudisha wakimbizi katika Taifa lake...


Rais wa Somalia ametaka kuwepo kwa njia muafaka ya kuwarudisha wakimbizii nchi kwake, huku Kenya ikisisitiza kuwa itaendelea na mpango wake wa kufunga kambi kubwa duniani.
Kambi ya Dadaab imekuwa kimbilio la wasomalia zaidi ya 300, 000.\
Rais Hassam Sheik Mohamed  ameiambia BBC  kuondolewa kwa lazima kwa wakimbizi hao haikuwa maslahi ya taifa lolote..
Kenya imesema inataka kufunga kambi kutokana na hali usalama, wakisema kuwa mashambulizi katika ardhi yao yamekuwa yakilengwa kwenye kambi hiyo..
Kenya haikutilia maanani vitisho vile vilivyo fanyika mwezi Aprili kufuatia mashambulizi ya vifo vya wanamgambo wa kundi la kisomali la Al- shabaab Kilomita 100 kutoka eneo la chuo..
Kundi la al-Qaeda linalohusishwa na mashambulzi hayo limekuwa likifanya mashambulio kadhaa nchini Kenya katika miaka ya hivi karibuni.
Akizungumza na BBC Rais Maohameid amesema kwamba, Uongozi unatakiwa kufanya makubaliano  katika kutafuta njia bora ya kuwarudisha watu hao katika taifa lao na katika hali inayoeleweka kulingana na sheria za kimataifa. Hatutaki mahusiano yetu yaathiriwe na Kenya,
Aliendelea kusema kuwa Kenya ilikuwa na msaada mkubwa katika kuwahifandhi wakimbizi kwa kipindi cha mda mrefu sasa na imekuwa ikijituma katika kuwarejesha watu wa taifa lake.
Daadab ilianzishwa mwaka 1991 kwa wanafamilia waliokuwa wakiikimbia Somalia kutoka na migogoro na baadhi ya watu wamekuwa wakiishi eneo hilo kwa zaidi ya miaka 20.

Related Posts

Rais Wa Somalia Ataka Njia Muafaka kuwarudisha wakimbizi katika Taifa lake...
4/ 5
Oleh
Show Comments: OR