Friday 10 July 2015

kituo cha polisi bunju cha chomwa moto kufuatia kifo cha mwanafunzi aliegongwa na gari na kupoteza maisha



siku ya leo eneo la bunju mkoani Dar es salaam kituo cha polisi ene la bunju kimechomwa moto baada ya gari kumgongwa mwanafunzi na kusababisha kifo chake na kusababisha barabara kufungwa kutokana na ajali hiyo.

baada ya ajali hiyo wanafunzi wa shule pamoja na wananchi waliamua kulala barabarani na kusababisha msongamano wa magari eneo hilo.
kituo kidogo cha polisi kikiwa kimechomwa moto
 
kwa sasa serikali  inawashikilia watu saba ambao walichoma kituo cha polisi pamoja na mwenyekiti ambae ndie aliwashinikiza wananchi kufanya vurugu hizo katika kituo cha polisi kufuatia kifo cha mwananfunzi huyo.
Moja ya gari binafsi ambalo lilichomwa moto na wananchi
kamanda wa polisi Suleiman Kova alisema kwamba kabla hajali hiyo ktokea dereva wa gari aina ya coster alimgonga mwananfuzi wa Bunju 'A'  kwa jina Radhia Omary katika eneo hilo na kusababisha kifo chake. na ndipo wananchi wakaamuaa kufanya mgomo na kufunga barabarani kwa saa tatu wakipiga kelele wakidai matuta ya wekwe ilikuepusha ajali katika eneo hilo ambalo liko karibu na shule hiyo. pia alisema kwamba mbali na kuchoma kituo cha polisi wananchi hao walifanya uharibifu katika magari manne ya watu binafsi yaliokuwa yameegeshwa pembezoni mwa kituo hicho.
Kituo vcha polisi kikiwaa kimechomwa moto
 
 
mda si mrefu polis waliwasili eneo hilo na kuwasambatatisha wananchi hao kwa kuiga risasi juu iliwaondoke barabarani.
bado polisi wanaenndelea  kumshikilia ereva wa gari aliemgonga motto huyo na bado wanaendelea kuwasaka wengine wlio husika katika kuchoma kituo hicho.

Related Posts

kituo cha polisi bunju cha chomwa moto kufuatia kifo cha mwanafunzi aliegongwa na gari na kupoteza maisha
4/ 5
Oleh
Show Comments: OR